TEEN TZ

BAADA YA ASLEY FELLA AMTOA MWANADADA

Miezi  kadhaa baada ya kumtoa  kumnawirisha  kimuziki 'bwamdogo'  Asley kutoka  mitaa ya Temeke jijini Dar, kampuni kubwa ya muziki wa  kizazi kipya Bongo, inayomiliki jina  la 'Mkubwa na Wanawe' sasa  iko tayari kumtoa mavumbini  na kumvisha ustaa wa muziki nchini binti mdogo  anayeitwa  Asna Juma 'Ching Chilla'.

Akizungumza na  Teentez.com  muda mfupi uliopita  'Big Bos' wa  kampuni hiyo  Said Fella Mkubwa Fella amefunguka kuwa  huu ni mwanzo wa mageuzi aliyopanga kuyafanya ndani ya muziki wa kizazi kipya kwa  kuwatoa nyota wa k*** ambao walikuwa ama hawapewi nafasi sana kama ilivyo kwa vijana wa kiume.

"Kwa mara ya kwanza tunamtoa msanii mdogo wa  k***, haya ni matunda ya mipango  iliyopo katika kampuni  yetu, kam ambavyo mnafahamu tumewatoa wengi lakini wote walikuwa ni wasanii wa kiume, safari  hii tumeamua kuweka nguvu kwa wasanii wa k*** na tutahakikisha wanapata mafanikio kama ambavyo wanapata wasanii wa kiume, hivyo nawaomba wadau wamsapoti binti huyu ambae tumeanza naye ili  kuweka  chagizo kwa wasichana wengine  kujitokeza  na hatimaye tukapata wanamuziki wengi wa k*** wenye mafanikio kam ailivyo huko kwa wenzetu. alisema Fella.

hapa chini ni video ya wimbo mpya wa  Ching Chilla  so cheki nayo halafu utasema nayo

STORI NA DISMAS TEN

Views: 444

Tags: AMTOA, ASLEY, BAADA, FELLA, MWANADADA, YA

Comment

You need to be a member of TEEN TZ to add comments!

Join TEEN TZ

Comment by renatus dominick on July 31, 2012 at 10:17am

Mkubwa na wanawe utaubeba mziki wa kibongo kwa kuwainua maandaground hapa bongo

Comment by ALLY YUSUPH on July 31, 2012 at 1:52am

mtoto ni mkali, level za akina Mwacti, lyna. wimbo huu kuna sehemu alitakiwa kupanda sana, kunung'unika sana lkn hajafanya. kiwango alichoonyesha akizoea atakuwa mkali Bigup!

© 2013   Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service