
Msanii wa Kigoma All Stars Chege Chigunda usiku wa jana amepata ajali mbaya ya gari maeneo ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Taarifa za awali kuhusu ajali hiyo zimesema kuwa usiku huo Chege alikuwa ametokea jijini Nairobi kwa shughuli kadhaa za kimuziki.
Katika mahojiano ya dakika chache na mtangazaji wa Clouds FM, Diva kwenye kipindi cha Ala za Roho, Chege amesema usiku huo wa saa nne akiwa kwenye gari alikutana pikipiki katika mtaa mmoja wa maeneo ya Temeke ambaye alimgonga na yeye kupata ajali hiyo , Chege amepata majeraha kadhaa lakini anaendelea vizuri licha ya gari lake kuharibika vibaya maeneo ya mbele.
Hivi ndivyo gari la Chege lilivyokuwa baada ya ajali
Haikuweza kufahamika mara moja hali ya mtu huyo aliyekuwa na pikipiki,Kupitia mahojiano hayo mafupi Chege amewatoa hofu mashabiki wake kuwa hali yake ni nzuri na yupo salama.
Staa wa bongo fleva Naseeb Abdul 'Diamond' amempa pole mwanamuziki mwenzie huyo wa Kigoma All Stars kwa kilichotokea na kuwataka wasanii wengine kumtia moyo Chege
"Nampa pole mwanangu Chege Chigunda kwa ajali mbaya ya gari aliyopata ,Tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote yaliyotokea" alisema Diamond.
STORI BY DISMAS TEN 0718489260
Comment
Comment by MOSES ANDERSON on September 2, 2012 at 10:53pm POLE SANA NAAMINI UTAPONA TU
Comment by DEOGRATIUS PAUL KESSY on August 6, 2012 at 10:43am da pole sana chegge usijali utapona
Comment by briannah meck on July 23, 2012 at 11:50am pole xana
Comment by Acleus K Tibaijuka on July 22, 2012 at 1:16am
Comment by Nasri Mussa on July 21, 2012 at 7:28am
Comment by Ally Said on July 18, 2012 at 1:39pm POLE SANA MTOTO WA MAMA SAID....2PO PAMOJA!!!!!!!!!!!!
Comment by Felix Salvatory Peter on July 18, 2012 at 4:21am Lkn leo nmemuona nyumban k-town na ametaambulishwa na mh ZITO kuwa ye nwanyumban kigoma. Pole sana jembe le2 la tmk wanaume.
Comment by kulwa yassin mitondwa on July 17, 2012 at 4:36pm pole sana mtu mzma.ajali hain kinga.....!!!!!!!
Comment by Joseph William Saghana on July 17, 2012 at 1:50pm pole kaka pamoja na wadau wote!!!!!!!
Hiphop staa wa Tanzania Albert Mangweha alifariki dunia akiwa Afrika Kusini May 28 2013 ambapo mpaka sasa chanzo cha kifo chake hakijajulikana na siku…
© 2013 Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.
You need to be a member of TEEN TZ to add comments!
Join TEEN TZ