TEEN TZ

KALAPINA AFUNGUKA KUHUSU UJIO WA RICK ROSS

Bosi wa  kundi mahiri la muziki wa  Hip hop hapa  Bongo, lijulikanalo kama  Kikosi cha Mizinga lenye maskani yake  pande za  Kinondoni jijini Dar, Kalama  Masoud Kalapina amesema  ujio wa  nyota wa muziki huo kutoka Marekani Rick Ross kwenye tamasha  la Fiesta  2012 ni zaidi ya  shoo kwa  wasanii wa  Tanzania.

Akizungumza  na teentz.com mapema leo Kalapina amesema kuwa  wasanii wa Bongo hawataakiwi kwenda  kwenye shoo ya  fiesta  kwa ajili ya kupiga picha na mkali huyo kwa ajili ya facebook na twitter  ama kwenda kugusa  tumbo kwani hazitawasaidia chochote kwenye muziki wao.

Hatutakiwi kwenda kwa ajiri ya facebook na twitter isipokuwa  tunatakiwa  kwenda kujifunza mbinu anazotumia kutawala jukwaa na pia kujaribu kuzungumza naye kuhusu njia ambazo anatumia  kupata mafanikio kimuziki na zaidi  kipi kimemfanya  kuwa mmoja ya mastaa walioleta mapinduzi kwenye muziki wa sasa  alisema Kalapina.

Akiendelea  zaidi Kalapina  alisema  kuwa  ujio wa Ross ni kitu  kikubwa sana  kwenye muziki wetu wa Tanzania na kutasaidia kwa kiasi kikubwa  kuitangaza  nchi yetu  hivyo anatoa  pongezi zote kwa  kampuni ya  Clouds Media kwa  kufanikisha  ujio huu.

Views: 753

Tags: AFUNGUKA, KALAPINA, KUHUSU, RICK, ROSS, UJIO, WA

Comment

You need to be a member of TEEN TZ to add comments!

Join TEEN TZ

Comment by Mkomwa Salum on October 12, 2012 at 1:19pm

its  true big bro umewachana afu inshu za playback hatuzimaind

Comment by emmanuel mushi on October 4, 2012 at 11:07am

dats true ma bwoy kalapna coz most of artist wanazani kuwa iyo ndo day yakutuuzia sura instead of learning and imitiating

Comment by emmanuel mushi on October 4, 2012 at 11:05am

dats true kalapina coz wasanii wetu wengi wanazani kuwa hiyo ndio siku ya kutuuzia sura

Comment by Innocent Quanama on October 2, 2012 at 3:53pm

that's good kamanda Kala Pina,,,

Comment by innocent kowe on September 30, 2012 at 2:14am
dat tru nigga w wnt 2 c changes bt I thnk itakuwa bonge moja la shoo
Bhaaaaaaaaaaaasssss

G5 CLICK - LATEST NEWS

LUDACRIS AACHIA MIXTAPE SIKU MOJA NA MOVIE ALIYOSHIRIKI "FAST AND FURIOUS 6"

Rapper LudaCris amedondosha moxtape yake mpya leo kupitia Datpiff.com ikiwa ni siku moja na release ya movie aliyoshiriki 'fast and furious 6', mixtape hiyo ina nyimbo10 na tayari ishadondoka leo hii, pichani ni cover yenye track list ya nyimbo hizo.…


 

© 2013   Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service