
SIYO filamu wala igizo, bali ni tukio la kweli lililozua hekaheka katika Kitongoji cha Shekilango, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo lililovuta umati mkubwa wa watu ambalo lilishuhudiwa na mwandishi wetu lilitokea Juni 6, mwaka huu saa 11:00 za jioni ambapo mke na mume walikimbizana wakitokea katika Nyumba ya Wageni ya A Plus Lodge, chumba namba 3 huku wakiwa watupu, Gazeti la Amani linakudadavulia kisa kizima.
Wakiwa wanakimbizana, mwanamke akiwa mbele alionekana kushikilia tumbo huku utumbo ukining’inia baada ya kudaiwa kuchomwa kisu na mwanaume huyo.
Mwanamke huyo aliyekuwa akipigania kuinusuru roho yake alikuwa akitoa maneno ya kuomba msaada kutoka kwa wasamaria wema akisema: “ Jamani nisaidieni, mume wangu anataka kuniua, anasema nimemsaliti.”
Hata hivyo, mwanamke huyo hakuweza kufika mbali kwani alianguka chini na baada ya sekunde chache akatokea mume wake, naye akiwa mtupu huku kisu kikiwa kinamning’inia tumboni baada ya kudaiwa kuwa alijichoma.
Muda mfupi baadaye askari wa jeshi la polisi walifika eneo la tukio na kuwachukua watu hao, wakawapeleka katika Kituo cha Polisi cha Urafiki na kufungua jalada la kesi namba URP/ RB/ 5126/2011 Mauaji.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camillus Wambura alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa bado wanalifuatilia na pia alithibitisha kifo cha mwanamke aliyemtaja kwa jina la Happy Samweli au Nyaso anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 27-30.
Polisi imegundua kuwa mke na mume hao waliingia katika nyumba hiyo Juni 5, mwaka huu asubuhi na mwanaume alijiandikisha kwenye daftari la mapokezi kwenye nyumba hiyo ya wageni kwa jina la Abdallah, mkazi wa Tabora.
Kwa mujibu wa Wambura, barua hiyo ilikuwa ikimlalamikia mwanamke huyo, Nyaso kuwa amemwambukiza ugonjwa wa Ukimwi na amegundua hilo baada ya kwenda kupima.
.
Source : Global PublishersComment
Comment by frank mibuli kilongola on July 27, 2011 at 4:13pm
Comment by DIARY on July 1, 2011 at 10:53am
Comment by Gabriel Kaliki on June 14, 2011 at 10:23pm
Comment by faudhiaomary on June 14, 2011 at 5:48pm
Comment by khalifalism on June 14, 2011 at 4:05pm
Comment by Karim Robert on June 13, 2011 at 1:15pm
Comment by Albert Lema on June 12, 2011 at 11:57am uyo mwananke ni evil.. she was supposed to be hanged...
Comment by Man Q on June 11, 2011 at 9:34pm Aiseeeeeee............??????????? It is veeeeeeeeeeeeeeeeeery Noma...!!!!!!
Daaaah.... Jamaa haangali hata alama za nyakati........anyway ni mtazamo wake..... I hope huo ndiyo mwisho wake wa kufikiria...... The guy does nat even get afraid from God.
Kweli NGOMA nooooooooooooooma kakma ndo hivyo.
© 2013 Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.
You need to be a member of TEEN TZ to add comments!
Join TEEN TZ