
NDOTO kufunga pingu za maisha siku za karibuni alizokuwanazo nyota kutoka 'Bongo moive' Hemed Suleiman 'PHD', zimeota mbawa kufuatia wazazi wa mlimbwende aliyetaka kumuoa kuweka ngumu.
katika mahojino ya dakika kadhaa aliyofanya na teentz.com, Hemed amesema kuwa tayari alikuwa ameanza taratibu za kushughulikia ndoa yake na mrembo huyo iliyopangwa kufungwa kimya kimya kwa kuogopa watu wenye nia mbaya lakini amejikuta akilazimika kustisha harakati hizo kufuatia wazazi wa binti huyo wakaweka ngumu kwa madai kuwa wanataka mtoto wao amalize kwanza masomo yake na kupata 'mastaz' kwa kuwa elimu ya Degree aliyonayo hivi sasa wanahisi bado haijamtosha.
"unajua mchumba wangu hivi sasa ana elimu ya degree hivyo wazazi wamesema kwao hiyo bado ni elimu ndogo hivyo hawezi kuruhusu jambo hilo kwanza mpaka apate 'mastaz' halafu ndiyo mambo mengine yatafuata, imeniuma sana kwa kuwa wenyewe tulishakubaliana na mwenzangu alikuwa tayari kwa hilo" alisema Hemed.
katika hatua nyingine Hemed ameiambia teentz.com kuwa yuko katika hatua za mwisho kutoa muvi yake mpya aliyoibatiza jina la Mererani ndani yake akiwa amemshirikisha swahiba wake wa kitambo Yusuf Mlela sambamba na wakali wengine kibao wanaofanya kweli na Bongo movie
wakati huo huo nyota huyo amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula tayari kwa ujio wa ngom ayake mpya iliyopewa jina la Mama Kimbo sambamba na video yake ambayo soon itakuwa hewani kupitia teentz.com.
STORI NA DISMAS TEN 0718489260
Comment
Comment by Juma Mdee on August 6, 2012 at 3:59pm Pole sana mdogo wangu,tambua hili,MJANJA WAKE MPUMBAVU. Elimu kitu gani dogo? Wangapi wameoa na wake zao wanaendelea na masomo? Huyo sio wako,geuka nyuma okota kijiti chapa mwendo.
Comment by Tumaini Chanyika on July 26, 2012 at 9:18pm no swagaz...........
Comment by briannah meck on July 23, 2012 at 11:49am don't worry meeen just be patience hopo yoyr wife will be good in education level as the way your good in musics ..big up dudie
Comment by Ivan Ian Ret on July 22, 2012 at 6:01pm
Comment by fadhili mpambya on July 21, 2012 at 11:53pm Bora kuoa bro kuliko kuzini mungu apendi bhanaa king of love
pole xana but mvumilivu hula mbivu dont pannic
Comment by Facejero Ismai on July 20, 2012 at 2:25pm
Comment by Ester Antapa on July 20, 2012 at 2:05pm mmh watu wanaolewa drsa la 7 sembuse degree? izo ni njama tu hemed we unadhani mzazi gani atakubali mwanae aolewe na msani ukampe presh mtoto wa wa2 na wazazi wake, tena ww???.. iyo ilikua kizuiz akuna cha masters apo we tafuta msani mwezio oa....
Comment by emmanuel mbaga on July 18, 2012 at 2:10pm KAKA UCKATE TAMAA KAMA UNAMPENDA KWELI VUTA SUBIRA MUDA UTAFIKA CHUKUA TOTOZ WEKA GETTO!!!!!!!!!!!!!!
Comment by Ally Said on July 18, 2012 at 1:35pm Ucjal jembe km kweli unampenda UTAMSUBILI...!!!!!!!!!!
Added by tanjin tareq on May 18, 2013
© 2013 Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.
You need to be a member of TEEN TZ to add comments!
Join TEEN TZ