

MSANII mahiri anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu bongo Rose Ndauka, asema kuwa baada ya kuwa kambini kwa muda mrefu akitengeneza kazi ambazo awali alizitaja sasa zimekamilika na Octoba zinaenda sokoni ambazo ni ‘Upofu’ na ‘Special Cover’ huku zote zikiwa zimefanyika chini ya kampuni yake inayojulikana kama Ndauka Entertainment.
Awali msanii huyo alisema kuwa filamu hizo zipo kwenye mchakato wa kupigwa picha lakini sasa ameamua kuweka wazi kuwa kila kitu kimekamilika na mwezi ujao zitakuwa sokoni kwa ajili ya kuwapa uhondo mashabiki.
Ndauka alisema kuwa ameamua kutoa filamu mbili kwa mpingo kwani mashabiki wake wana hamu ya kuona kazi nyingi zaidi na nzuri kutoka kwenye kampuni yake pia malengo yake ni kujitangaza zaidi kimataifa.
“Nakumbuka niliwahi kusema Octoba nitakuja na filamu mbili kutoka kwenye kampuni yangu kazi zipo tayari hivyo kinachosuburiwa ni ratiba ifike ili mashabiki wangu waweze kuona utamu wa kazi zangu, ujio huo utakuwa ni mzuri kwani utaifanya kampuni yangu iweze kujulikana zaidi kimataifa,” alisema.
Comment
tuna isubili kwa hamu sana
Comment by shitabo on September 27, 2012 at 4:10pm
Comment by Sunday Komu on September 26, 2012 at 2:26pm Added by tanjin tareq on May 18, 2013
© 2013 Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.
You need to be a member of TEEN TZ to add comments!
Join TEEN TZ