TEEN TZ

Mwigizaji ‘five star’ kutoka tasnia ya filamu Bongo, Jacqueline Wolper Masawe, amenyang’anywa ‘mkoko’ (gari) wa kifahari aliokuwa akitanua nao katika mitaa ya mbalimbali ya jiji la Bongo.

Habari zenye ukweli 100% ambazo Teentz.com imezinyaka zinasomeka kuwa Wolper anayejulikana kama Amber Rose wa Bongo amenyang’anywa mkoko huo aina ya BMW X6 wenye thamani ya ‘ngawira’ za kibongo ML 170, sambamba na kupigwa ‘stop’ kukaribiana na mshefa aliyekuwa amemnunulia ndinga hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo, hatua ya mshefa huyo kuamua kuchukua ndinga yake ni baada ya kugundua kuwa Wolper anatoka kimapenzi na ‘sharobaro’ mmoja anayemiliki duka maarufu la viwalo pande za Kinondoni.

Aidha chanzo hicho, kimeieleza Teentz.com kuwa hivi sasa mwanadada huyo ameamua kutembelea ndinga aina ya Noah aliyokuwa anaitumia hapo awali sambamba na kutoka kwa kuvizia kukwepa watu wake wa karibu washitukie mchongo.
Katika kuhakikisha kuwa ukweli unajulikana Teentz.com iliamua kumsaka na baada ya kupatikana Wolper aligeuka mbongo na kudai kuwa hakuna jambo kama hilo isipokuwa kilichotokea ni kuwa gari limepata matatizo na ameamua kulipeleka ‘garage’.

Alipotakiwa kueleza kuwa imekuwaje gari mpya kama ile aipeleke garage tene kwa siku tatu Wolper alisme hivi: “Bwana eeh wee jua liko ‘garage’ hayo maswali mengine mimi sitaki kuayasikia na kama una taka ugomvi endelea kuniuliza” alisema na kuondoka haraka eneo alilokuwa amekaa

……………………………………Stori na Dismas Ten………………………………

Views: 3863

Tags: ANYANG’ANYWA, GARI, WOLPER

Comment

You need to be a member of TEEN TZ to add comments!

Join TEEN TZ

Comment by Fanuel Machumu on July 13, 2012 at 10:58pm

Heyi madada ze2 kwanini msiwe mnapewa na card za hayo magari, kelele nyingi kumbe mnakimbiza upepo

 

Comment by Erick Kibada. on July 1, 2012 at 6:28pm

Huruama

Comment by prince muni khan on June 28, 2012 at 6:58pm

tatizo la mademu wa kibongo ni was****ge

Comment by fadhili mpambya on June 28, 2012 at 12:13pm

kweli mapenzi jau!

Comment by Mussa Jacob on June 26, 2012 at 3:33pm
Tatizo la dada zetu ndo Hilo hawawezi kutulia na 1, kabisaaa.
Comment by stephen mwanyonga on June 25, 2012 at 10:16pm

titi for tat iz a fair game,,,, ye kamwona sharobaro ndo wa maana so mshefa amefanya right decision..........

Comment by josephine john on June 22, 2012 at 2:44pm

teh teh aya cyakwetu macho namackio

Comment by man.dume02 on June 20, 2012 at 3:26pm

NDIYO AKOME CHA MTU MAVI

Comment by Hashim Ramadhani Makusi on June 20, 2012 at 2:12pm

Tutafahamu ukweli tu! Time will tell.

Comment by Wilson Obeid Chishomi on June 19, 2012 at 6:03pm

SUPER STAR WA BONGO

G5 CLICK - LATEST NEWS

Advertisement

Latest Activity


 

© 2013   Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service