TEEN TZ

Photos

Loading…
  • Add Photos
  • View All

Music

Loading…

Advertisement

 

Videos

  • Add Videos
  • View All
 

Members

Advertisement

Blog Posts

UPDATES VURUGU MTWARA:ENEO LILILOTENGWA KUJENGWA VIWANDA LINATEKETEA KWA MOTO

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 7:04pm 0 Comments

Eneo lililotengwa kwa ajili ya viwanda likiteketea kwa moto. Eneo liko karibu na bahari. Lilikuwa linamilikwa na serikali na ujenzi chini ya kampuni kutoka Marekani ulikuwa unaendelea. Wazungu wamekusanya baadhi ya vitu vyao na kuondoka eneo hilo.

VURUGU MTWARA;SPIKA MAKINDA AAHIRISHA KIKAO CHA BUNGE JIONI HII

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 6:38pm 1 Comment



Spika ameahirishwa bunge hadi kesho kutokana na hali ya Mtwara.

Spika kasema amepokea hali ya vurugu mtwara, hivyo bunge limeahirishwa ili kutoa fursa kwa kamati ya bunge kujadili suala hilo na serikali imetakiwa kutoa majibu katika kikao cha kesho.

Spika kasema kuwa wabunge wangependa kujadili hali ya Mtwara leo lakini watajadili nini wakati hata wao wabunge wamepata taarifa hizo kwenye vyombo vya habari? Hivyo, akaiagiza serikali kuleta majibu sahihi kesho bungeni na kuwaomba wabunge kuwa na subira hadi kesho na kisha akaahirisha bunge. Akahitimisha kwa kusema kamati ya bunge inakwenda kujadili suala hilo sasa…

BREAKING NEWZ:MTWARA HALI BADO TETE

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 5:04pm 0 Comments

Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo. Jengo moja ambalo linadaiwa kuwa ni ofisi ya CCM ya saba saba mkabala na chuo cha TIA limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa. Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) imechomwa moto. Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.
TEENTZ inaendelea kukupa update kwa kila kitakachoendela,stay visting

AZAM KULETA BOTI MPYA YA KISASA

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 4:30pm 0 Comments

Kampuni ya Azam Marine inatarajia kuleta boti mpya ya kisasa itakayoitwa Kilimanjaro 4,nchini, kuanzia ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 700 na kutumia muda wa dakika 70 kwa safari moja ya kati ya Zanzibar na Dar es Salaam. boti hii itakidhi mahitaji ya wasafiri wa eneo hili kwa kuwa inabeba sifa zote, ambazo ni Usalama, Kasi zaidi na Unadhifu. Kilimanjaro 4 itaingia mwishoni mwa mwezi huu wa 5

BREAKING NEWS: MTWARA KIMENUKA

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 3:30pm 0 Comments

Habari zilizotufikia kutoka Mtwara zinaeleza kuwa kumeibuka vurugu ambazo zimepelekea mabomu ya machozi na risasi za moto kutumika baada ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kusomwa bungeni na kueleza kuwa mradi wa gesi Mtwara utatekelezwa bila kutaja faida za moja kwa moja watakazozipata wananchi hao.…

DIAMOND NA NAY WA MITEGO KUPAMBANA TENA NDANI YA MAISHA CLUB

Posted by Teen Newz on May 22, 2013 at 2:00pm 0 Comments

Baada ya mpambano kufanyika Dar live kumtafuta nani anafanya mziki wa kweli between hip hop na wale mchele mchele(bongo fleva)na kukosekana mshindi ishu nzima inahamia Maisha club,show ikiwa tofauti kabisa na zilizopita,hapa kutakuwa na black carpet kwa Hip hop wakiongozwa na Nay wa mitego,pembeni white carpet kwa wana bongo fleva wakiongozwa na the president,Diamond platnumz.
kiingilio na mda vyote vinasomeka kwenye picha hapo juu,na kama jadi yetu,TEENTZ tutakuwa wa kwanza kukuletea picha yote ya kilichofanyika,Stay visting

Advertisement...

 
 
 

© 2013   Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service