
Staa wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ amevuta mkoko wa Kijanja wenye thamani ya ‘mkwanja wa Kibongo Milioni 60 keshi.
Akizungumza na Teentz.com muda mfupi baada ya kupokea ‘dinga’ hiyo aina ya Land Cruiser Prado TX kutoka kwa wakala aliyekuwa akishughulikiwa mpango mzima wa kuingia kwake hapa Bongo, Diamond alifunguka kuwa alikuwa na mpango wa kuvuta mkoko ‘dizaini’ hiyo kitambo lakini kuna mambo kadhaa yakawa yanachelewesha.
“Nashukuru Mungu kuwa mpango wangu umetimia, nilipanga hivi kitambo lakini kuna baadhi ya mambo yalichelewesha hatua hiyo, najua watu watasenama mengi kuhusu hili lakini ukweli ni kuwa huu ni mchuma wangu” alisema Diamond.
Katika hatua nyingine Diamond alifunguka kuwa awali alinunua mdinga kama hiyo huko visiwani Zanzibar, lakini baada ya kuikagua aligundua kuwa lina matatizo na kuamua kulirudisha na kuagiza kitu kipyaaaaaa.
Kwa habari zaidi unaweza kucheki ..www.thisisdiamond.com
Comment
Comment by john jeremiah on August 5, 2012 at 9:49am mmmmmmmmmmmmmmh cio kiiini macho icho
Comment by EMMANUEL FRANK on July 8, 2012 at 11:20am wasafi classic.........halah........inaumaaaaa......lingine lini .....ila inaummmaaaaaaaaaaaaa....cong......
Comment by Sharobaro Shababi on June 26, 2012 at 10:01am Ebhana jembe zaiiiidiii....Haaaallllllah!!!!!!!!
Comment by husein m. pima on June 25, 2012 at 11:54pm aiseee jombaa hiyo ni poa sanaa tu kitu cha TX
Comment by nasser i milulu on June 25, 2012 at 7:50pm mimi nakupongeza sana tena sana bt remember ii ni bongo,wapi MR nice alikuwa kama ivyo leo kiko wapi??
Comment by nasser i milulu on June 25, 2012 at 7:45pm hongera mdogo wangu,but jok....t hakufai
mkubwa umetisha kinomer nomer kwa hiyo ndinga............
so, hapo heshimu mziki kama ndo kazi yako kiongozi !!!
byeeee !!!
Comment by Prince Quizo on June 24, 2012 at 2:22pm big up mzazi kwa kujivutia kitu kama hicho lazima wema azidi kupagawa
Comment by rajabu tamambele on June 23, 2012 at 5:57pm hongera yake hayo ni matunda ya kazi zake big up
Comment by KIJAZI wa KIJAYO on June 23, 2012 at 5:11pm kumbuka ulipotoka acha mambo ya kuiga hii ni tanzania kunamengi ya kufanya!! majigambo ya nn kunamengi ya kufanya kwa uwo mkwanja ulio nunulia ndinga....... na jamii ikafaidika na mchango wako 4example hospital na n.k
© 2013 Designed & Developed by G5 CLICK COMPANY.
You need to be a member of TEEN TZ to add comments!
Join TEEN TZ